Mkuu wa mkoa wa Arusha Magesa Mulongo amesema wasaudi wanne waliokamatwa kuhusiana na shambulio hilo waliwasili katika uwanja wa ndege wa Arusha siku ya Jumamosi, na kwamba Watanzania wanne waliokamatwa ni wakristu, lakini hakutoa maelezo zaidi. Balozi wa Vatican nchini Tanzania Francisco Montecillo Padilla, alikuwa akihudhuria misa katika kanisa hilo ambalo limejengwa upya, lililoko katika viunga vya jiji la Arusha, lakini hakudhuriwa.
Maafisa hawajatoa ishara zozote kuhusiana na nani aliefanya shambulio hilo, lakini wasiwasi umekuwa ukiongezeka kati ya jamii za Wakristu na Waislamu katika miezi ya hivi karibuni. Rais Kikwete amewataka Watanzania kuwa watulivu wakati polisi ikiendelea na uchunguzi wake.
chanzo:dw
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Post a Comment
Post a Comment