MAHAKAMA ya Wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya imewahukumu kutumikia kifungo cha maisha jela vijana wawili wakazi wa wilayani Chunya mkoani humo kutokana na kosa la ubakaji wa mwanamke mmoja waliyemtendea kitendo hicho mbele ya watoto wake.
Kadhalika, mahakama hiyo imewahukumu vijana hao wawili kutumikia kifungo cha miaka 30 jela kutokana na kosa la unyang’anyi wa kutumia silaha ambapo siku ya tukio walimjeruhi mume wa mwanamke waliyembaka.
Vijana waliokumbwa na vifungo hivyo viwili kutokana na mashitaka mawili yaliyokuwa yakiwakabili ni Ngaru Joseph (32) na Pili Mneme Kapigi (30) wote wakiwa ni wakazi wa wilayani Chunya mkoani Mbeya.
Awali ilielezwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashitaka wa Jeshi la Polisi Mazoya Luchagula, Mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo Alice Mkasela kuwa mnamo Julai 10, mwaka huu saa nane usiku nyumbani kwa mlalamikaji katika Kijiji cha Ukwavila wilayani Mbarali washitakiwa walivamia na kuvunja mlango nyumba ya mkazi huyo aliyekuwa amelala na mke na watoto wao.
Luchagula alisema walipofanikiwa kuingia ndani ya nyumba hiyo washitakiwa hao walimjeruhi baba wa familia kwa kumkata na shoka kichwani kisha wakapora fedha kiasi cha Sh 580,000, wakachukua nguo zote za wanafamilia na kisha kumbaka mama wa familia mbele ya mumewe na watoto.
Mwendesha mashitaka huyo alisema wanafamilia hao kupitia mwanga wa taa ya sola waliweza kuwatambua watuhumiwa kabla wazazi hawajapelekwa Hospitali ya Misheni Chimala walikolazwa kwa ajili ya matibabu.
Kutokana na makosa hayo Luchagula aliiomba Mahakama kutoa adhabu kali kwa washitakiwa ili iwe fundisho kwa watu wengine walio na tabia hizo wilayani hapa na kwingineko nchini.
Akito adhabu kwa washitakiwa, Hakimu Mkasela alisema ameridhishwa na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo na pande zote mbili na kwamba kwa kosa la kwanza la unyangaji wa kutumia silaha washitakiwa watakapaswa kutumikia kifungo cha miaka 30 jela na kwa kosa la pili la ubakaji watatumikia kifungo cha maisha jela ili iwe fundisho kwao na watu wengine.
Awali washitakiwa waliiomba Mahakama kuwapunguzia adhabu wakisema bado umri wao ni mdogo na wanategemewa na familia zao, maombi ambayo yalitupiliwa mbali na hakimu Mkasela.
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Je Umezisoma Hizi?
- Tetemeko Lililotokea Jana Katika Mikoa Ya Kanda ya Ziwa Limeua Zaidi ya Watu 10 na Kujeruhi Wengine 12011 Sep 20160
Tetemeko la ukubwa wa mtikisiko wa kipimo cha Ritcher 5.7 limetokea katika mikoa mitatu nc...Read more ?
- Msafara wa Makamu wa Rais, Samia Suluhu wapata ajali Mtwara.09 Sep 20160
Msafara wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani, Mama Samia Suluhu Hassan ambao uliku...Read more ?
- Polisi Washuhudia Majambazi Yakitwangana Risasi.......Zakamatwa Shehena za Silaha na Vifaa vya Uhalifu06 Sep 20160
WATU watatu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi wa kutumia silaha, ambao wamehusika kufanya matukio ...Read more ?
- Askari Magereza Atiwa Mbaroni Kwa Kuingia Wodini Akiwa Amelewa na Kisha Kuanza Kufyatua Risasi28 Aug 20160
POLISI mkoani Rukwa inamshikilia askari Magereza, Cleophas Chapaulinge kwa kosa la kulewa na k...Read more ?
- Polisi Mwingine Auawa Kwenye Mapambano Makali na Majambazi Huko Mkuranga27 Aug 20160
Ilikuwa ni kama filamu ya askari na maadui wakati askari wa Jeshi la Polisi walipopambana na wat...Read more ?
- RC Makonda: Polisi Mkikuta Mtu Yeyote Msituni Pigeni bila Huruma.......Haki za binadamu Wakiwauliza Waambieni waje Kwangu26 Aug 20160
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ameliagiza Jeshi la Polisi kuwagonga na kuwapiga wah...Read more ?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Post a Comment