Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Leo Shujaa mkubwa wa Yanga alikuwa Mchezaji wa Burundi Amisi Tambwe aliepachika Bao 4 huku Simon Msuva akipiga Bao 2 na nyingine kufungwa na Mchezaji wa Liberia, Kpah Sean Sherman, likiwa Bao lake la kwanza kwenye Ligi, na jingine na Salum Telela.

Amisi Tambwe amefunga manao manne Yanga ikishinda 8-0 leo dhidi ya Coastal Union Ligi Kuu.

Sherman amefuta mkosi kwa kutoa pasi za mabao matatu na kufunga bao moja.

Nao Azam FC, wakiwa kwao Azam Complex huko Chamazi kwenye Viunga vya Jiji la Dar es Salaam, walipiga mkenge baada ya kutoka Sare ya Bao 1-1 na Mbeya City inayopigana kujinusuru kutokumbwa na balaa la kushuka Daraja.

Azam FC walitangulia kufunga kwa Bao la Kipre Balou Dakika ya 61 lakini Dakika 4 baadae Mbeya City walisawazisha kwa Penati ya Raphael Alpha.

Matokeo ya Leo yamewafanya Yanga SC wawe juu zaidi kileleni wakiwa na Pointi 43 kwa Mechi 20 na Azam FC wakibaki Nafasi ya Pili wakiwa na Pointi 37 kwa Mechi 19.  

VINARA wa Ligi Kuu Vodacom Yanga SC Leo April 8, 2015 , wameitekeza Coastal Union Bao 8-0 Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam na kupaa kileleni wakiwa Pointi 6 mbele ya Mabingwa Watetezi Azam FC ambao nao Leo nao wamekwaa mkenge wa Mbeya City baada kutoka nao Sare ya Bao 1-1.

 Huko Uwanja wa Taifa ilikuwa burudani tupu kwa Washabiki wa Yanga ambao Wikiendi iliyopita walisheherekea Timu yao kutinga Raundi ya Pili ya Mashindano ya CAF ya Kombe la Shirikisho baada ya kuibwaga FC Platinum kwa Jumla ya Mabao 5-2 katika Mechi mbili.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top