Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Tevez aliwakusanya ndugu, jamaa na marafiki na kufanya dua hiyo, Ijumaa iliyopita nyumbani kwao Msamvu, Madawa jirani na Shule ya Msingi Msamvu ‘A’ ambapo alifanya kisomo hicho kilichoambatana na dua na chakula.

“Mungu amemnusuru na balaa lile, amemkingia hivyo ameona ni vyema aandae dua ya kumshukuru,” alisikika mmoja wa waalikwa.Baadhi ya mashehe na waumini wengine wa Kiislamu waliohudhuria dua hiyo walimpongeza Tevez kwa kitendo hicho cha kumkumbuka Mungu na kumshukuru kwa kumlinda na majanga yaliyomkuta.

“Hili ni jambo jema sana alilofanya Tevez ambapo tunaelekezwa na mitume wetu kwamba tumshukuru Mungu kwa kila jambo,” alisema mmoja wa waumini wa dini ya Kiislamu.Kwa upande wake Tevez alisema amamshukuru Mungu kwani amempigania sana uhai wake.

“Lilikuwa  ni tukio kubwa kwangu, sikutegemea kama ningenusurika, Mungu amenipigania sana nimeona bora nijumuike na ndugu, jamaa na marafiki kumshukuru Mungu,” alisikika Tevez.Januari mwaka huu, Tevez alitekwa na watu wasiojulikana katika mji wa Durban nchini Afrika Kusini ambapo mwenyewe alibainisha kuwa mwenyeji wake mjini humo alivujisha habari kuwa ana fedha ndipo akavamiwa, akateswa na kuporwa fedha na simu zake mbili

Tevez aliwafungulia mashtaka vijana waliohusika na tukio hilo ambapo kesi inaendelea kuunguruma nchini humo.
GPL

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top