Umati wa abiria wakiwa kwenye kituo cha daladala cha Darajani-Ubungu huku kukiwa hakuna daladala yoyote inayofanya kazi baada ya kutokea kwa mgomo wa madereva wa Daladala jijini Dar.
Baadhi ya abiria wakiwa wamepanda magari ya mizigo baada ya kukosekana kwa daladala maeneo yote ya jiji la Dar es Salaam leo asubuhi.
Mmoja wa abiria akiongea na dereva wa kibasi kidogo kuangalia kama kuna uwezekano wa kupata usafiri maeneo ya Mwenge jijini Dar.
Katika kituo cha mabasi cha Mpakani eneo la Mwenge zilionekana Bajaj zikipakia na kushusha abiria baada ya madereva kuingia kwenye mgomo leo asubuhi.
Habari toka Morogoro zinaarifu kuwa Abiria wamejazana katika vituo vya daladala, bodaboda ndo zinatoa msaada (kwa wale wenye uwezo).
Mdau Toka Kahama anaarifu kuwa mpaka sasa hakuna basi hata moja lililotoka kwenda mikoani.
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Post a Comment
Post a Comment