Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Msanii wa filamu Bongo, Fatuma Ayubu ‘Bozi’ amesema kuwa migogoro yote inayomtokea aliyewahi kuwa mwandani wake, Emmanuel Elibariki ‘Nay’ ni kutokana na laana ya kumsambazia picha zake za utupu.

Akiongea  na  mwandishi wetu, Bozi alisema tatizo kubwa lililomkuta Nay kwa mpenzi wake Siwema kumfumania na njemba ni malipo ya kupuuza penzi lake na dhambi kubwa aliyomtendea ya kusambaza picha zake za utupu alizomtumia wakati walipokuwa kwenye uhusiano.

“Nilimpenda mno Nay lakini fadhila ya penzi langu akaona anidhalilishe kwa kuanika picha zangu za utupu kwenye mitandao ya kijamii,  jambo linalonisononesha mpaka kesho, naamini yaliyomtokea ni laana yangu anayotembea nayo kwani bado sijamsamehe kwa kitendo kile cha ajabu alichonifanyia,” alisema Bozi.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top