Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Hofu‬ imewakumba waumini wa ‪Kanisa‬ ‪Katoliki‬ la Mtakatifu Stephano, ‪‎Kisarawe‬ mkoani ‪‎Pwani‬ katika ibada ya Ijumaa Kuu baada mtu mmoja kukamatwa katikati ya ibada ya Ijumaa Kuu akiwa na bastola yenye risasi nane.

Kwa mujibu wa habari zilizopatikana kutoka kwa waumini na kuthibitishwa na polisi, mwanaume huyo ambaye si muumini wa kanisa hilo anadaiwa kutaka kufanya uhalifu kanisani hapo na alikamatwa baada ya waumini kushtukia mienendo yake isiyo kuwa ya kawaida.

Tukio hili limetokea katika kipindi ambacho kuna tishio la uhalifu unaohusishwa na ‪‎ugaidi‬ katika maeneo mbalimbali nchini, ambapo kuna uporaji wa silaha unaofanywa na watu wasiojulikana baada ya kuwaua polisi.
 
Vilevile tukio hili limetokea wakati waumini hao hawajasahau mauaji ya kutisha nchini ‪Kenya‬ ambako magaidi wamevamia Chuo Kikuu cha ‪‎Garissa‬ na kuua wanafunzi 147.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top