Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Mrembo na Staa wa Bongo Fleva, ambae nyota na jina lake lilianza kusikika Kupitia shindano la Bongo Star Search (BSS), Meninah La Diva amesema angekuwa na uwezo angewapatanisha mastaa wawili wa Bongo Movies , Wema Sepetu na Kajala Masanja ambao alisema kuwa anawependa sana.

Meninah aliyasema hayo leo alipokuwa akifanya mahojiano na mtangazaji Millard Ayo kwenye c kipindi cha Amplifaya, alipoulizwa kuwa angekuwa na uwezo angewapatanisha mastaa gani ambao wamegombana au hawaelewani kwa namna moja au nyingine.

“Ningekuwa na uwezo ningewapatatinisha Wema na Kajala kwasababu wote nawapenda”-Meninah alijibu

Wema na Kajala walikuwa marafiki wa karibu lakini urafiki wao ulivunjika na kwasasa sio marafiki tena.

Hakika wengi tunapenda wawili hawa waelewane na urafiki  wao urudi, wewe je?

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro
18 Mar 2015

Post a Comment

 
Top