Mastaa wawili wa Bongo Fleva, Menina Atick na Baba Levo wamenaswa kimahaba hivyo kuibua viulizo kuwa huenda kuna ‘projekti’ inaendelea kati yao.
Katika tukio hilo ambalo Baba Levo alishuhudiwa ‘akijibebisha’ kwa Menina lilijiri kwenye Ukumbi wa Escape One, Mikocheni jijini Dar ambapo wawili hao walijumuika na wasanii wenzao katika hafla ya uzinduzi wa Kampeni ya Ishi Kistaa iliyokuwa ikichukua nafasi ukumbini hapo.
Wakati burudani na mambo mengine yote yakiendelea mahali hapo, Baba Levo na Menina walijitenga wakaenda kubana chobingo na kuanza kufanya yao.
Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi
Post a Comment
Post a Comment