Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Mrembo na mwigizaji  wa filamu, Blandina Chagula ‘Johari’ amekiri kwamba wakati anaingia kwenye uhusiano wa kimapenzi na nyota wa fani hiyo, Vincent Kigosi ‘Ray’ alijua yupo na nguli wa filamu, Ruth Suka ‘Mainda’.
Johari alikili hayo Katika mahojiano mafupi na Gazeti moja la udaku siku ya Jumanne jijin Dar, mahojiona yalikuwa hivi.
Mwandishi: “Kwanza napenda kujua kama kweli umerudiana na Ray maana kuna minong’ono kwamba penzi lenu kama zamani.”
Johari: “Siyo kweli. Kwanza mimi sipendagi hayo maswali miaka yote mambo ni hayohayo, sasa nimekua mtu mzima na mambo lazima yabadilike.”
Mwandishi: “Kwa hiyo huna uhusiano na Ray?”
Johari: “Sina.”

Mwandishi: “Sasa kama ni kweli mbona ofisi yako bado ipo nyumbani kwa akina Ray? (Sinza-Mori).”
Johari: “Kazi zinakwenda kama kawaida. Mimi na Ray kwenye kazi hatuna tatizo lolote, asubuhi nafungua ofisi baadaye watu wanakwenda ‘lokesheni’.”
Mwandishi: “Hebu niambie kuhusu Mainda. Wakati unaingia kwenye uhusiano na Ray ulijua kuna Mainda?”
Johari: “Ndiyo nilijua.”

Mwandishi: “Ikawaje ukaingia sasa?”
Johari: “Hilo swali silitaki.”
Mwandishi: “Oke, je wewe na Mainda mna mawasiliano mazuri?”
Johari: “Yes! Ikibidi kuwasiliana tunawasiliana, tuko sawasawa.”

Mwandishi: “Inasemekana umefunga pub yako ya kuuza pombe, ni kweli?”
Johari: “Ilibidi nifunge, mwenye nyumba alisema hapendi niuze pombe pale, natafuta sehemu nyingine.”
Mwandishi: “Nashukuru sana Johari.”
Johari: “Poapoa.”

GPL

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top