August 12, 2025 08:05:05 AM Menu
 

Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Kijana mmoja shija kasamwa mwenye umri wa miaka 28,leo mchana amejikuta akipata masahibu ambayo iwapo atapona kamwe hatayasahau kabisa ktk maisha yake.

Kijana huyo mkazi wa mkoa wa Shinyanga ktk kijiji cha Chela ameng'atwa na nyoka mwenye sumu kali akiwa msituni akivunja amri ya sita na mke wa mtu.

Inasemekana ndio ilikuwa tabia yake kufanya uchafu huo na mwanamke huyo asiye mwaminifu ktk ndoa yake.

Sasa leo kama kawaida yao walijirusha msituni,wakiwa huko kabla hawajaanza kufanya mapenzi walisikia sauti za watu wakija upande waliokuwepo ndipo wakaamua kuingia kichakani kwa hofu ya kuonekana,ndani ya kile kichaka kikubwa kilichokuwa kimefungasha miti mingi kiasi kwamba haikuwa rahisi kuonekana kwao,ndipo wakaamua kufanya uchafu wao eneo hilo ndipo wakiwa bado wanaendelea na starehe ilihali yule kijana akiwa kashusha suruali yake na makalio yake kubaki wazi alishtuka ghafla kang'atwa na nyoka huyo anayesadikiwa kuwa ni aina ya cobra,kelele za maumivu zikakusanya wanakijiji na mke wa mtu akakimbia kwa hofu.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro
22 Feb 2015

Post a Comment

 
Top