Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

MSIKIE kiungo wa Yanga, Andrey Coutinho, anachosema kwamba anafurahishwa na mfumo wa sasa wa timu yao chini ya kocha Hans Van Der Pluijm kwani unamfanya aonekane bora uwanjani tofauti na alipokuwa chini ya Mbrazili mwenzake, Marcio Maximo.

Coutinho aliliambia Mwanaspoti kuwa soka la kuzuia wakati wa Maximo lilikuwa linampa tabu na hakuufurahia mfumo huo tofauti na sasa ambapo amepewa uhuru wa kucheza kwa kushambulia.

Alisema hakuwa na amani wakati Yanga ilipokuwa chini ya Maximo kwani alikuwa anajua safari ya kurudi kwao Brazil inaweza kumkuta muda wowote kwa kuwa angeonekana wa kawaida uwanjani kama ilivyokuwa kwa Genilson Santos ‘Jaja’ ambaye pia aliponzwa na mfumo wa kuzuia.

“Sikuwahi kufurahia soka wakati nipo na Maximo hapa Yanga, kwani tulikuwa tunacheza kwa kuzuia na sikupata muda mwingi wa kushambulia kwa uhuru na kazi ilikuwa kubwa ya kushuka kuzuia na wakati huohuo mpandishe mashambulizi,” alisema.
Chanzo:Mwanaspoti

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro
07 Jan 2015

Post a Comment

 
Top