
Msanii maarufu wa filamu nchini King Majuto amesema kuwa ana nia ya kufanya filamu ya pamoja na Wema Sepetu na Diamond Platnumz.
Akizungumza na Bongo5, King Majuto ambaye filamu zake nyingi zinafanya vizuri sokoni alisema kuwa amekutana na Wema hivi majuzi na kumueleza hilo na kumtaka azungumze kuhusu project hiyo ili Diamond akikubali wafanye kazi pamoja.
Ingawa uwezo wa Diamond katika filamu bado haujulikani lakini kama mastaa hao wote watu wakiwa ndani ya filamu moja na kupata msambazaji mzuri na mkweli ni lazima wafaidike kwa mauzo makubwa ya filamu hiyo.
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro







Post a Comment
Post a Comment