Watu
walioishi katika ndoa kwa miaka 62 wamekufa pamoja nchini Marekani. Don
na Maxine Simpson, kutoka Bakersfield, California walipishana kwa saa
chache tu kufa, katika vitanda vilivyowekwa karibu, huku wakishikana
mikono katika saa zao za mwisho duniani.
Melissa
Sloan, ambaye ni mjukuu, amesema bibi yake alitangulia kufa, na mwili
wake ulipoondolewa chumbani, babu yake naye akafuata.

"Kitu pekee alichokitaka Don ni kuwa na mke wake mpenzi. Alimpenda sana bibi yangu, mpaka mwisho”
Don alikuwa na umri wa miaka 90, huku Maxine akiwa na miaka 87. Walikutana mwaka 1952 na kuoana mwaka huohuo.

Wawili
hao waliwahi kuishi nchini Ujerumani wakati Don akifanya kazi katika
jeshi la Marekani kama mhandisi, na walipokuwa huko, wali-asili watoto
mapacha wa kiume kutoka katika nyumba moja ya kulelea watoto yatima.
Waliporejea Marekani, Maxine alifanya kazi ya uuguzi huku Don akifungua kampuni yake ya uhandisi.
Wameacha mtoto mmoja wa kiume na wajukuu watano
UKIONA TUKIO LOLOTE LINATOKEA USISITE KUTUTUMIA PICHA KUPITIA WHATSAPP 0712-483 331
kama huja like ukurasa wetu wa facebook fanya hivi sasa ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu bonyza hapaFacebook Blogger Plugin by Kibonajoro







Post a Comment
Post a Comment