
Mtumoja
ambaye hajatambulika amekutwa ameuwawa kwa kuchomwa chomwa sehemu
mbalimbali za mwili wake na kitu chenye incha kali katika makaburi ya
misuna Singida mjini.
Wakielezea
tukio hilo balozi wa mtaa wa mwenge Bi. Mary Mwambusu na mwenyekiti wa
mtaa wa misuna Bwana Sarota Masawe wamesema tukio hilo linaonekana
kutokea majira ya alfajiri ya siku ya tarahe tano mwezi wa nane katika
makaburi ya misuna.
Viongozi
hao wa mtaa Mwenge na Misuna wamesema tukio hilo ni la kwanza kutokea
lakini wameliomba jeshi la polisi kuimarisha ulinzi hasa maeneo kama
hayo ilikudhibiti mauaji kama hayo yasi tokee tena.
Akiongea
kwa njia ya simu kamanda wa jeshi lapolisi mkoani Singida Bwana Geofrey
Kamwela amekiri kutoke kwa tukio hilo katika eneo la makaburi yaliyopo
misuna Singida mjini na amesema jeshi lake bado linaendelea na uchunguzi
kuweza kubaini chanzo cha mauaji hayo ambayo ni ya kinyama.
UKIONA TUKIO LOLOTE LINATOKEA USISITE KUTUTUMIA PICHA KUPITIA WHATSAPP 0712-483 331
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro







Post a Comment
Post a Comment