
Na Baraka Mpenja,
RAIS
mstaafu wa klabu bya Simba sc, ambaye ni mbunge wa Tabora Mjini, Ismail
Aden Rage imelazwa Hospitali ya mkoa wa Dodoma baada ya kupata ajali ya
gari akitokea Tabora kueleka mjini Dodoma leo.
Imeelezwa kuwa Rage alikuwa anakwenda Dodoma kuhudhuria vikao maalumu vya bunge la katiba.
Ajali hiyo imetokea eneo la Chigongwe mkoani Dodoma.
Ajali hiyo imetokea eneo la Chigongwe mkoani Dodoma.
Imeripotiwa
kuwa katika gari hilo, Mheshimiwa Rage alikuwa na abiria wengine ambao
ni mbunge wa viti maalumu, Munde Tambwe, Issa Chimwaga , Mwanahamisi
Ramadhani na Dereva John NKoya.
Abiria wote walipata majeruhi, isipokuwa dereva wa gari hilo, lakini wanaendelea kupata matibabu na hali zao zinakwenda vizuri.
Rage
amezungumza akiwa wodini mkoani Dodoma, na kueleza kuwa amepata
majeraha katika bega la mkono wa kushoto na eneo la nyuma ya mgongo.
Rage
aliongeza kuwa ajali hiyo imetokea wakati dereva wa gari lao akijaribu
kulipita roli, lakini ghafla dareva wa Roli hilo akaingia katikati ya
barabara na ikamlazimu dereva wao kwenda pembeni ya barabara na gari
kupinduka na kutumbukia kwenye korongo.
Mtandao huu unafuatilia taarifa kamili kuhusu ajali hiyo.
Ugua pole mwanamichezo Rage na abiria wengine wote.
Ugua pole mwanamichezo Rage na abiria wengine wote.
UKIONA TUKIO LOLOTE LINATOKEA USISITE KUTUTUMIA PICHA KUPITIA WHATSAPP 0712-483 331
kama huja like ukurasa wetu wa facebook fanya hivi sasa ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu bonyza hapa
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro







Post a Comment
Post a Comment