Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This


Watoto wawili mapacha waliozaliwa wakiwa wameungana tumbo na kifua, wamefariki muda mchache baada ya kuzaliwa katika kituo cha afya Katoro wilaya ya Geita mkoani Geita. Akizungumza, mama wa watoto hao, Neema Luswetura (23), alisema alijifunga Agosti 6, muda mchache baada ya kufikishwa katika kituo hicho cha afya. 
Muuguzi  wa zamu katika kituo hicho, Joyce Michael akizungumza na mwandishi wa habari hizi, alisema walimpokea mwanamke huyo saa 7 usiku akilalamika uchungu, na hivyo kupelekwa wodi ya wazazi na asubuhi alijifungua watoto wenye uzito wa kilo 5.1 wakiwa  wameshikana na kufariki. 


Alisema wakati wa zoezi la kumzalisha, alilazimika kuomba  msaada toka kwa mganga wa zamu, Dk. Daniel Izengo ili kunusuru uhai wa mama huyo lakini watoto wake hawakuweza kupona. 
Dk. Izengo alithibitisha kuwepo kwa tukio hilo na juhudi za kunusuru uhai wa watoto hao zilishindikana, akieleza kitalaam tukio hilo linajulikana (coujoined twins). 
Kutokana na hali hiyo, Dk. Izengo ameishauru jamii hususani wajawazito kuzingatia ushauri wanaopewa  na madaktari.
UKIONA TUKIO LOLOTE LINATOKEA USISITE KUTUTUMIA PICHA KUPITIA WhatsApp:- 0712483331.

 
Like ukurasa wetu wa facebook  ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu bonyza hapa

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top