
Wananchi wakitolea kuchimba kaburi.

Askari wa
jeshi la zimamoto na uokoaji Iringa wakijianda kuopoa mwili wa kijana
kutoka mto Ruaha karibu na darajani eneo la Ipogoro, Manispaa ya Iringa.

Gari la zimamoto likijiandaa kuondoka baada ya kumaliza kazi.
Na Friday Simbaya, Iringa
WAKAZI wa
Manispaa ya Iringa walijitokeza kwa wingi katika mto Ruaha mdogo
kushuhudia mwili wa kijana wa jinsia ya kiume ukiwa umeelea juu ya maji
ya mto huo huku Jeshi la Zima moto na Uokoaji kwa kushirikiana na Jeshi
la Polisi mkoani hapa kuuopoa mwili ukiwa umeharibika vibaya.
Baada ya
jeshi la uokozi kuopoa mwili huo waliuweka pembeni ya mto huo na kisha
kuukabidhi kwa jeshi la polisi kwa ajili ya kuufanyia uchunguzi.
Kijana huyo ambaye hakufahamika kwa jina wala makazi yake alizikwa kandokando ya mto. huo baada ya kukosekana kwa ndugu zake.
Akithibitisha
kutokea kwa tukio hilo kamanda wa polisi mkoani iringa Ramadhani Mungi
alisema kuwa tukio hilo lilitokea jana majira ya saa 10:00 Jioni eneo la
ipogoro lililopo ndani ya manispaa ya iringa.
Kamanda
mungi alisema kuwa mwili wa marehemu ulikutwa ukiwa hauna nguo huku
akibainisha kuwa marehemu anakadiriwa kuwa na umri wa kati ya miaka 20
hadi 30.
Baada ya
kuopolewa kwa mwili huo polisi kwa kuyshirikiana na jeshi la uokozi
pamoja na vikosi vya ulinzi waliitisha mkutano wa utambuzi ili kama
atajuikana aweze kuchukuliwa na ndugu zao lakini hakuna hata mmoja
aliyejitokeza.
Hata hivyo polisi hao waliiamua kuzika mwili huo pembezoni mwa mto huo huku mwili huo ukiwa umeharibika vibaya.
"Ni kweli
tulipata taarifa kutoka kwa wasamaria wema na tulifika eneo la tukio na
hatimaye kwa kushirikiana na jeshi la uokozi tulimuokoa japo kijana
huyo hakuweza kufahamika jina wala kabila na sisi polisi hatuna taarifa
yeyote ya mtu kupotea."alisema mungi
Wakati
huo huo mashuhuda waliliambia MJENGWABLOG kuwa kitendo cha jeshi hilo
kuzika mwili huo pembezoni mwa mto huo sio vizuri kutokana na mto huo
kutumiwa na wakazi wengi wa manispaa ya iringa.
Mashuhuda
hao ambao hawakupenda majina yao yaandikwe walisema kuwa jeshi hilo
lisingetakiwa kuzika eneo hilo badala yake wangetafuta eneo lingine kwa
ajili ya maziko licha ya mwili huo kuwa umeharibika.
UKIONA TUKIO LOLOTE LINATOKEA USISITE KUTUTUMIA PICHA KUPITIA WHATSAPP 0712-483 331
kama huja like ukurasa wetu wa facebook fanya hivi sasa ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu bonyza hapa
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro







Post a Comment
Post a Comment