Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This


Navas: Mungu amesikia kilio changu cha muda mrefu
Mlinda mlango kutoka nchini Costa Rica, Keylor Antonio Navas Gamboa, amesema amefurahishwa na hatua ya kusajiliwa na klabu kubwa duniani ambayo alikuwa na ndoto za kuitumikia siku moja katika maisha yake.
Navas amesema anaamini dua na sala ambazo kila leo alikuwa akiomba kwa mungu wake, ndizo zimemfikisha hapo alipo na kilichobaki ni kujitahidi na kujiahakikishia nafasi katika ushindani wa kukaa langoni kwa msimu ujao wa ligi.

Amesema kitendo cha viongozi wa klabu ya Real Madrid kukubali kumsajili na kisha kumsainisha mkataba wa miaka sita, kinampa fikra za kujiamini na kutarajia makubwa kutoka kwenye klabu hiyo inayoushikilia ubingwa wa barani Ulaya kwa sasa.
"Mungu amesikia maombi yangu, amenisaidia na amenionyesha njia ya kufika nilipokuwa napahitaji kila siku, nitajitahidi kufanya kila niwezalo ili niendelee kuzisogelea ndoto za maisha yangu ya soka.”
"Mkataba wa miaka sita si haba, ni mkataba wa muda mrefu sana, unanipa mwanga na kuamini nitakuwa hapa kwa kipindi kirefu zaidi ambacho nitatakiwa kuonyesha ushupavu na ukamilifu wangu wote pale nitakapopata nafasi ya kuwa langoni mwa Real Madrid." Amesema Navas
Hata hivyo mlinda mlango huyo mwenye umri wa miaka 27, amewataka mashabiki wake kuwa wastahamilivu katika kipindi hiki ambacho anatarajia kuwa katika hatua tofauti na alivyokuwa mwanzo.
UKIONA TUKIO LOLOTE LINATOKEA USISITE KUTUTUMIA PICHA KUPITIA WHATSAPP 0712-483 331


kama huja like ukurasa wetu wa facebook fanya hivi sasa ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu bonyza hapa

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top