
Mlinda
mlango kutoka nchini Costa Rica, Keylor Antonio Navas Gamboa, amesema
amefurahishwa na hatua ya kusajiliwa na klabu kubwa duniani ambayo
alikuwa na ndoto za kuitumikia siku moja katika maisha yake.
Navas
amesema anaamini dua na sala ambazo kila leo alikuwa akiomba kwa mungu
wake, ndizo zimemfikisha hapo alipo na kilichobaki ni kujitahidi na
kujiahakikishia nafasi katika ushindani wa kukaa langoni kwa msimu ujao
wa ligi.
Amesema
kitendo cha viongozi wa klabu ya Real Madrid kukubali kumsajili na
kisha kumsainisha mkataba wa miaka sita, kinampa fikra za kujiamini na
kutarajia makubwa kutoka kwenye klabu hiyo inayoushikilia ubingwa wa
barani Ulaya kwa sasa.
"Mungu
amesikia maombi yangu, amenisaidia na amenionyesha njia ya kufika
nilipokuwa napahitaji kila siku, nitajitahidi kufanya kila niwezalo ili
niendelee kuzisogelea ndoto za maisha yangu ya soka.”
"Mkataba
wa miaka sita si haba, ni mkataba wa muda mrefu sana, unanipa mwanga na
kuamini nitakuwa hapa kwa kipindi kirefu zaidi ambacho nitatakiwa
kuonyesha ushupavu na ukamilifu wangu wote pale nitakapopata nafasi ya
kuwa langoni mwa Real Madrid." Amesema Navas
Hata
hivyo mlinda mlango huyo mwenye umri wa miaka 27, amewataka mashabiki
wake kuwa wastahamilivu katika kipindi hiki ambacho anatarajia kuwa
katika hatua tofauti na alivyokuwa mwanzo.
UKIONA TUKIO LOLOTE LINATOKEA USISITE KUTUTUMIA PICHA KUPITIA WHATSAPP 0712-483 331
kama huja like ukurasa wetu wa facebook fanya hivi sasa ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu bonyza hapa
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro







Post a Comment
Post a Comment