Moja
kati ya mambo ambayo mtu wa anayafikiria kabla hajanunua gari ni kiasi
cha mafuta kinachotumiwa na gari hilo. Lakini ukiwa na gari hili…
unaweza usifikirie kabisa kuhusu mafuta huku ukilitumia kama kawaida kwa
zaidi ya miaka 100.
Wataalam
wa masuala ya magari wameeleza kuwa endapo gari linalotumia ‘Thorium’
litaanza kufanya kazi litakuwa gari ambalo linaweza kutumika kwa zaidi
ya miaka 100 bila kuongezwa mafuta.
Kwa maana hiyo Thorium itakuwa na uwezo wa kudumu hata zaidi ya maisha ya mtumiaji wa gari hilo.
Kampuni
ya Laser Power tayari imeshatengeneza idea ya kutumia Thorium katika
engine za magari ambapo wataitumia kitaalam kuchemsha maji na kuwa
chanzo cha nguvu ya kuendesha gari.
Hata
hivyo, CEO wa Laser Power System, Dr. Charles Sevens aliiambia Mashable
kuwa engine za Thorium hazitaweza kuwa kwenye magari hivi karibu kwa
kuwa watengenezaji wa magari hawataki kuzinunua.
Cars are not our primary interest. The automakers don’t want to buy them.” Alisema Dr Charles Stevens.
Alisema
makampuni mengi ya magari yanataka kutengeneza pesa zaidi kwa kutumia
engines za gas na kwamba itawachukua miongo kadhaa kukubali na kuanza
kutmia teknolojia ya Thorium
Endapo
gari hili litafanikiwa kuingia sokoni na kununuliwa na watu wengi miaka
ijayo, itakuwa hatari kwa biashara ya mafuta hasa kwa wale wanaotegemea
magari pekee kufanya mauzo.
UKIONA TUKIO LOLOTE LINATOKEA USISITE KUTUTUMIA PICHA KUPITIA WHATSAPP 0712-483 331
kama huja like ukurasa wetu wa facebook fanya hivi sasa ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu bonyza hapa
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Post a Comment
Post a Comment