Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Baada ya kukatika kwa umeme majira ya saa moja na dakika shirini na tatu na kusababisha karibu mikoa yote ambayo imeunganishwa na Gridi ya taifa kukosa nishati ya umeme na kusimamisha shughuli za bunge ikiwemo zoezi la upigaji wa kura ya bajeti ya serikali, 
 
mkurugenzi mtendaji wa shirika la umeme nchini Tanesco mhandisi Felchesim Mramba ametoa afafanuzi juu ya kukatika huko kwa umeme na kubainisha kuwa mafundi wa shirika hilo wanaendelea kufanya uchunguzi nini kimesababisha tatizo la kukatika kwa umeme na kusababisha usumbufu kwa wateja wa Tanesco.

Amesema hali hiyo imetokana na kuzimika ghafla kwa mitambo na kusababisha nchi nzima kuwa gizani,ambapo chanzo cha kuzimika kwa mitambo hiyo bado hakujajuliana.

Amesema kikubwa kinachofanyika sasa ni kurejesha huduma wakati uchunguzi ukiendelea kufanyika

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top