Baada ya kukaa hopitalini kwa muda wa miezi sita akiwa amepoteza fahamu (coma), dereva wa mbio za magari ya formula 1 ambaye ni mshindi mara saba Michael Schumacher ameruhusiwa kutoka katika hospitali ya Grenoble University, Ufaransa.
Schumacher ametoka katika hospitali nchini Ufaransa na ameelekea Uswizi ambako atakuwa anapatiwa matibabu chini ya uangalizi wa watu wake wa karibu na madaktari binafsi.
Akizungumzia hali yake ya afya, meneja wake Sabine Kehm amethibitisha kuwa Schumacher yuko katika hali nzuri kiasi lakini ameshatoka kwenye coma.
Schumacher alipata alilazwa hospitalini hapo tangu December 29 mwaka jana baada ya kupata ajali katika milima ya barafu alipokuwa akitereza kama sehemu ya mchezo.BONYEZA HAPA
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro







Post a Comment
Post a Comment