Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
David Luiz


Chelsea wamekubali kumuuza beki David Luiz kwa takriban paundi milioni 40 kwenda kwa mabingwa wa Ufaransa Paris St-Germain.
Luiz alijiunga na Chelsea kutoka Benfica Januari 2011 kwa paundi milioni 21.3.
"Uhamisho huo sasa unasubiri David Luiz kukubaliana masuala binafsi na PSG na pia kufanyiwa vipimo vya kiafya" imesema taarifa kwenye tovuti ya Chelsea.
Luiz amekuwa akinyatiwa na Barcelona kwa misimu miwili iliyopita, lakini PSG wameamua 'kuvunja benki' na kumfanya beki aghali zaidi duniani.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top