Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Mchezaji Sylvain Azougoui alifariki uwanjani baada ya kupiga teke ya kichwani
Mchezaji wa klabu ya Ac Bongoville,Sylvain Azougoui amefariki baada ya kupigwa teke ya kichwani wakati wa mechi ya ligi kuu nchini Gabon.

Kipa huyo alifariki alipokuwa akipelekwa hospitalini baada ya tokeo hilo wakati wa mechi yao dhidi ya klabu ya Centre Mberi Sportif.

Kipa huyo mwenye umri wa miaka 30 kutoka Togo alikuwa amelisimamisha kombora lililopigwa langoni mwake, lakini mshambulizi alipoteza mwelekeo na kumkanyaga Azougoui kichwani.

Mechi hiyo ya siku ya Jumapili ilichezwa Bongoville ambalo liko umbali wa kilomita 800 kutoka Libreville mji mkuu wa Gabon.

"Ni vigumu sana kushuhudia hali hii ya uchungu ,'' ilisema taarifa katika mtandao wa klabu hiyo.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top