Polisi mjini Musoma wametumia mabomu ya machozi kudhibiti ghasia zilizoibuka, baada ya wafuasi wa Chadema kupambana na mbunge wa zamani wa Musoma Mjini, Vedastus Mathayo.
Walifanya fujo juzi jioni baada ya mjumbe huyo wa Halmashauri Kuu ya CCM
(NEC) kudaiwa kuingilia safari ya Katibu Mkuu wa Chadema Dk. Willbroad
Slaa ya kwenda kwenye msiba wa Sheikh wa Mkoa wa Mara Athumani
Mageyee.
Hata hivyo, kabla ya kufika msibani, Mathayo alijitokeza kuelekea
nyumbani kwa Sheikh huyo na kuwalazimisha wafuasi wa Chadema waliokuwa
wameusindikiza msafara wa Dk. Slaa, kupanga mawe barabarani kumtaka
asubiri.
Wakizungumza kwa jazba wakiwa wanapanga mawe hayo, walisema mbunge huyo
wa zamani ni mwenyeji wa Musoma lakini tangu msiba utokee hajawahi
kuhani lakini alipoona viongozi wa Chadema wanakwenda naye
akajitokeza.
“Tunashangaa huyu Mathayo kuja kwenye msiba baada ya kuona viongozi wa
Chadema wanakwenda wakati yeye ni mwenyeji na hajawahi kukanyaga, sisi
tunaamini hakuwa na lengo zuri na ndiyo tukamzuia,” alisema Jacob
Mwita.
Ghasia hizo zilisababia polisi kulifika eneo la vurumai na kuwatawanya
kwa kupiga mabomu ya machozi, hali hiyo ilidumu kwa muda wa nusu saa na
kusababisha baadhi ya wafuasi wa Chadema kuwashambulia polisi.
Kufuatia hali hiyo, Mbunge wa sasa wa Jimbo hilo, Vincent Nyerere ,
alilazimika kuingilia kati kuwatuliza wafuasi wa Chadema waliokuwa
wanaendelea kupambana na polisi.
CHANZO:
NIPASHE
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Post a Comment
Post a Comment