Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This


Polisi mjini Musoma wametumia mabomu ya machozi kudhibiti ghasia zilizoibuka, baada ya wafuasi wa Chadema kupambana na mbunge wa zamani wa Musoma Mjini, Vedastus Mathayo.
Walifanya fujo juzi jioni baada ya mjumbe huyo wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) kudaiwa kuingilia safari ya Katibu Mkuu wa Chadema Dk. Willbroad Slaa ya kwenda kwenye msiba wa Sheikh wa Mkoa wa Mara Athumani Mageyee.

Kiongozi huyo alikwenda kuhani msiba wa Sheikh huyo aliyefariki wiki hii.
 
Hata hivyo, kabla ya kufika msibani, Mathayo alijitokeza kuelekea nyumbani kwa Sheikh huyo na kuwalazimisha wafuasi wa Chadema waliokuwa wameusindikiza msafara wa Dk. Slaa, kupanga mawe barabarani kumtaka asubiri.

Wakizungumza kwa jazba wakiwa wanapanga mawe hayo, walisema mbunge huyo wa zamani ni mwenyeji wa Musoma lakini tangu msiba utokee hajawahi kuhani lakini alipoona viongozi wa Chadema wanakwenda naye akajitokeza.

“Tunashangaa huyu Mathayo kuja kwenye msiba baada ya kuona viongozi wa Chadema wanakwenda wakati yeye ni mwenyeji na hajawahi kukanyaga, sisi tunaamini hakuwa na lengo zuri na ndiyo tukamzuia,” alisema Jacob Mwita.

Ghasia hizo zilisababia polisi kulifika eneo la vurumai na kuwatawanya kwa kupiga mabomu ya machozi, hali hiyo ilidumu kwa muda wa nusu saa na kusababisha baadhi ya wafuasi wa Chadema kuwashambulia polisi.

Kufuatia hali hiyo, Mbunge wa sasa wa Jimbo hilo, Vincent Nyerere , alilazimika kuingilia kati kuwatuliza wafuasi wa Chadema waliokuwa wanaendelea kupambana na polisi.

CHANZO: NIPASHE

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top