MGANGA wa kienyeji ‘Sangoma’aitwaye Ramadhani Issa (20) amedaiwa
kuwatorosha watoto wawili, Salim Swalehe(13) na Laurent Oscar (13)
wanaosoma katika Shule ya Msingi ya Pamba jijini hapa.
Sangoma Ramadhani Issa (20) akiwa chini ya ulinzi baada ya kunaswa.
Inadaiwa kwamba watoto hao walirudi makwao kwa njia za ajabu na kusema walikuwa wamewekwa ndani kama misukule nyumbani kwa mganga huyo.
Watoto waliokuwa wametekwa na sangoma Ramadhani Issa.
OFM wakiwa na mtandao wa kijamii wa Farijika, waliambiwa na watoto hao kwamba walichukuliwa na mganga huyo Desemba 27, mwaka jana wakiwa katika matembezi ya sikukuu.
“Mganga alitugusa na shanga vichwani na kutufanya tupoteze kumbukumbu na kumfuata kila alipokuwa akienda,” alisema Laurent.
Hapa ni ndani ya getho la Sangoma Ramadhani Issa walipokuwa wakiishi watoto.
Kama haitoshi walidai mganga alikuwa akiwalimisha na kuwachotesha michanga usiku kucha huku Salim akionesha chale alizochanjwa sehemu za magotini na kichwani.
Mtoto Salim alisema kuwa alimuona mwenzake Laurent akiruka kimiujiza jambo lililomshtua na kumfanya atoroke baada ya kumuona mganga huyo kauacha mlango wazi.
“Ndani ya nyumba kuna mauzauza mengi sana, wakati mwingine tulikuwa tunasikia sauti za watoto lakini hatukuwaona.
“Hata chakula (karanga na ulezi) tulikuwa tukipewa kingi, lakini tukila kidogo tu kinaisha kama vile tulikuwa tunakula na watu wengine,” alisema Salim.
Mmoja wa wazazi wa watoto hao ambaye ni Makamu wa Rais wa Chama cha Waganga wa Tiba za Jadi Tanzania (Tameto), Swalehe Issa Bukuku, alisema kuwa watoto hao walifika nyumbani wakiwa katika hali ya kuweweseka huku wakisisitiza walikuwa kwa mganga Igogo na wangeweza kuwapeleka kwa kuwa wanaikumbuka njia waliyopita siku ya kwanza.
OFM na wazazi wa watoto hao pamoja na wanaharakati walifika kwa mganga huyo wakiwa na mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Ujaluoni.
Bahati mbaya mganga huyo alikuwa ametoka hadi ndugu yake alipompigia simu na kumtaka afike kilingeni baada ya kuambiwa kulikuwa na wateja.
Mganga huyo alifika kilingeni kwake ndipo OFM ikiwa pamoja na mwenyikiti wa mtaa na wazazi wa watoto hao na Polisi Jamii, walimnasa na kumfikisha Kituo Kikuu cha Polisi cha Nyamagana na kufunguliwa jalada la uchunguzi MW/RB/07/2014 JALADA LA UCHUNGUZI.
Mganga huyo alidai kwamba hakuwaiba watoto hao bali aliwachukua ili wamsaidie kazi ya kumlisha paka wake huku akikana kuwachanja na kuwafanyisha kazi usiku.
-OFM via GPL
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro







Post a Comment
Post a Comment