Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
                      dkMakamu wa Rais Dk. Mohamed Gharib Bilal ndio alikua mgani rasmi katika mashindano hayo ya uhuru marathonmar
Mbio za kuienzi siku ya Uhuru wa hapa nchini zilifanyika siku ya jana ya tarehe 8, ambapo ilijumuisha washiriki mbalimbali katika mashindano hayo. Mbio hizo zilianzia katika viwanja vya leaders na kumalizkia hapo hapo, mashindano hayo yalijumuisha urefu wa KM42 kwa mbio ndefu na KM21 kwa mbio fupi.

Katika mbio za kilomita 42 kwa upande wa wanaume mshindi alikuwa ni Jamini Ikai kutoka nchini Kenya, akifuatiwa na Steven Sylvester wa Tanzania na nafasi ya tatu ilishikwa na Alex Sanka kutoka Tanzania.
Kwa upande wa wanawake nafasi ya kwanza ilichukuliwa na Thabita Kibeti wa Kenya, akifuatiwa na Naumi Jepkosgei wa Kenya na nafasi ya tatu ikachukuliwa na Banuelia Brighton wa Tanzania.

Kwenye mbio za kilomita 21 upande wa wanaume nafasi ya kwanza na ya pili ilichukuliwa na Elijah Tirop pamoja na Wilson Tuitoe nafasi ya tatualichukua Eliah Daudi wa Tanzania.

Kwa upande wa wanawake nafasi ya kwanza ilikamatwa na Jacqueline Juma wa Tanzania na Angela Temu wa Kenya alitwaa nafasi ya pili na nafasi ya tatu alichukuwa Catherine Range wa Tanzania.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top