MKUU wa Wilaya ya Mvomero (DC), Antony Mtaka amezusha tafrani na
kulalamikiwa na baadhi ya wanachama wa Jumuiya ya Wanawake Tanzania
(UWT), wilayani humo baada ya kutoa kauli kwamba wasikubali kutumika
kama kondomu ama tambara la deki wakati wa chaguzi mbalimbali.
Wakizungumza na wandishi wa habari mjini hapa, wanachama hao ambao
hawakupenda majina yao yaandikwe gazetini, walisema mkuu huyo wa wilaya
alitoa kauli hiyo wakati wa kikao cha Baraza la UWT ambacho kilifanyika
Desemba 12 mwaka huu kwenye ofisi za CCM Dakawa wilayani humo.
Walidai kuwa kiongozi huyo alialikwa kwenye baraza hilo na baada ya kupewa nafasi ya kuzungumza na wajumbe, aliwaambia maneno hayo kwa maelezo kuwa kuna wanasiasa wanaowania nafasi mbalimbali wilayani humo, wakati wa uchaguzi huja kujipendekeza.
“Kwa kweli kauli alizotuambia mkuu wetu wa wilaya si nzuri, zimetusikitisha…kutufananisha na kondomu na tambara la deni? Ametukosea kwa kweli, sisi ni watu wazima, hakupaswa kutufananisha na vitu hivyo,”alisema mmoja wa akina mama hao.
Akijibu tuhuma hizo mkuu huyo wa wilaya alikiri kutumia kauli hizo na kudai kuwa hakuwa na nia mbaya kama wao walivyofikiria isipokuwa hizo ni siasa chafu za baadhi ya wanasiaa wa Mvomero.
“Mwandishi sikiliza, hizo zote ni siasa chafu za Mvomero, ni kweli nimewaambia hivyo kwa sababu tunahitaji michango ili jumuiya hiyo iendelee na kama kuna aliyeguswa awasaidie. Hebu fikiria kuna viongozi wangapi wilayani kwetu, lakini hakuna hata mmoja aliyewachangia ingawa wamewapelekea barua, ila ikifika mwakani wakati wa uchaguzi utawaona wakiwaendea, ndiyo maana nimewaambia hivyo,” alisema.
Akimtetea mkuu huyo wa wilaya, Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Mvomero, Rachel Kingu alisema kiongozi huyo aliwaambia wanaUWT hivyo kwa sababu wilaya hiyo imekuwa na wanasiasa wenye siasa za uchochezi na kuwataka wanachama wake kuwa makini.
Credit: GPL
![]() |
| Mkuu wa Wilaya ya Mvomero (DC), Antony Mtaka. |
Walidai kuwa kiongozi huyo alialikwa kwenye baraza hilo na baada ya kupewa nafasi ya kuzungumza na wajumbe, aliwaambia maneno hayo kwa maelezo kuwa kuna wanasiasa wanaowania nafasi mbalimbali wilayani humo, wakati wa uchaguzi huja kujipendekeza.
“Kwa kweli kauli alizotuambia mkuu wetu wa wilaya si nzuri, zimetusikitisha…kutufananisha na kondomu na tambara la deni? Ametukosea kwa kweli, sisi ni watu wazima, hakupaswa kutufananisha na vitu hivyo,”alisema mmoja wa akina mama hao.
Akijibu tuhuma hizo mkuu huyo wa wilaya alikiri kutumia kauli hizo na kudai kuwa hakuwa na nia mbaya kama wao walivyofikiria isipokuwa hizo ni siasa chafu za baadhi ya wanasiaa wa Mvomero.
“Mwandishi sikiliza, hizo zote ni siasa chafu za Mvomero, ni kweli nimewaambia hivyo kwa sababu tunahitaji michango ili jumuiya hiyo iendelee na kama kuna aliyeguswa awasaidie. Hebu fikiria kuna viongozi wangapi wilayani kwetu, lakini hakuna hata mmoja aliyewachangia ingawa wamewapelekea barua, ila ikifika mwakani wakati wa uchaguzi utawaona wakiwaendea, ndiyo maana nimewaambia hivyo,” alisema.
Akimtetea mkuu huyo wa wilaya, Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Mvomero, Rachel Kingu alisema kiongozi huyo aliwaambia wanaUWT hivyo kwa sababu wilaya hiyo imekuwa na wanasiasa wenye siasa za uchochezi na kuwataka wanachama wake kuwa makini.
Credit: GPL
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro








Post a Comment
Post a Comment