Kwa mujibu wa baadhi ya wakazi wa jijini hapa, hali imekuwa tofauti
na matukio mengine kwani askari wamekuwa wengi wakihakikisha wanawanasa
watuhumiwa waliohusika katika tukio hilo.
“Mwanza haikaliki, kila kona askari wametapakaa na baadhi ya watu wanakimbia mji hadi suala hili litakapopoa,” alisema mmoja wa wakazi wa jijini hapa.
Mabina ambaye aliwahi kuwa Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Mwanza aliuawa na wanakijiji baada ya kudaiwa kumuua kwa kumpiga risasi mtoto mwenye umri wa miaka 11.
Wanakijiji wa Kanyama walitumia silaha za jadi kumshambulia Mabina hadi alipofariki dunia alipokuwa akipanda miti na kutengeneza njia kwa ajili ya kupitisha trekta lake kwenye ardhi yenye mgogoro.
“Mwanza haikaliki, kila kona askari wametapakaa na baadhi ya watu wanakimbia mji hadi suala hili litakapopoa,” alisema mmoja wa wakazi wa jijini hapa.
Mabina ambaye aliwahi kuwa Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Mwanza aliuawa na wanakijiji baada ya kudaiwa kumuua kwa kumpiga risasi mtoto mwenye umri wa miaka 11.
Wanakijiji wa Kanyama walitumia silaha za jadi kumshambulia Mabina hadi alipofariki dunia alipokuwa akipanda miti na kutengeneza njia kwa ajili ya kupitisha trekta lake kwenye ardhi yenye mgogoro.
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro








Post a Comment
Post a Comment