
Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe
*Asema anajipanga kwenda kortini
*Amwandikia Dk. Slaa kudai kauli ya Chadema
NAIBU Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Zitto Kabwe, ameibuka na kutoa kauli na tamko dhidi ya tuhuma mpya dhidi yake zilizosambazwa katika mitandao ya intaneti katika siku za hivi karibuni.
Zitto, ambaye pia ni Naibu Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni na Mbunge wa Kigoma Mjini, amefanya hivyo akitumia majukwaa mawili tofauti. Mwanasiasa huyo kijana ambaye amejipambanua kuwa mtetezi wa misingi ya utaifa, raslimali za nchi, uchumi na masuala ya utawala bora ndani na nje ya chama chake, alifanya hivyo kwa mara ya kwanza juzi jioni, wakati alipokuwa akihutubia mkutano mkubwa wa hadhara katika uwanja wa Kolimba wilayani Kariua, Mkoa wa Tabora.
“Katika umri huu mdogo, nimepigwa mishale mingi ya kisiasa, mimi ni binadamu nina damu, nikipigwa hii mishale damu inatoka, ninaumia, sasa nimechoka kupigwa mishale, lazima sasa tuambiane ukweli,” alisema Zitto.
Saa kadhaa baada ya hotuba yake hiyo, Zitto ambaye kwa muda mrefu sasa amekuwa katika mzozo wa wazi na baadhi ya viongozi wenzake ndani ya Chadema, alisambaza tamko la maandishi ambalo lilibeba ujumbe unaofanana na ule alioutoa Kariua.
Awali katika mkutano wa Kariua, Zitto alisema alikuwa hayuko tayari kuendelea kukaa kimya pasipo kuchukua hatua zikiwamo za kisheria wakati akichafuliwa.
Alisema alikuwa ameshamwandikia barua Katibu Mkuu wake, Dk. Wilibrod Slaa, akihoji iwapo taarifa ya kumchafua iliyosambazwa katika mitandao ya intaneti chini ya kiichwa cha habari kisemacho “Taarifa ya Siri ya Chadema” ni ya chama hicho au la.
Zitto aliyekuwa akizungumzia matokeo ya ziara yake ya kufuatilia kuhusu fedha zilizofichwa na baadhi ya Watanzania katika mabenki ya Uswisi na kwingineko Ulaya, alieleza kusikitishwa na kile alichodai kuwa ni kikundi cha watu ndani ya Chadema ambacho kimekuwa mstari wa mbele kumpaka matope.
story kamili Bofya hapa
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro







Post a Comment
Post a Comment