
Wahamiaji wakiokolewa kutoka baharini
Maafisa katika kisiwa kikubwa
cha Sicily katika bahari ya meditarenia wanasema kuwa wamepata maiti 82
baada ya meli iliyokuwa imewabeba takriban wahamiaji 500 wa kiafrika
kushika moto na kuzama katika kisiwa cha Lampedusa.
Shughuli kubwa ya uokozi inaendelea kuwatafuta manusura.
Meya wa mji huo anasema kuwa walionusurika wako hatika hali ya mshutuko na walimwambia kuwa moto mdogo uliwashwa baada ya meli kukwama na lengo lilikuwa kuitisha msaada.
Lakini alisema kuwa moto ulisambaa kupita kiasi na ikawa vigumu kuudhibiti.
Kisiwa cha Lampedusa kiko kati ya Tunisia na Sicily na kimekuwa kiingilio kikuu cha wahamiaji kuingia barani Ulaya.
----bbc
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro








Post a Comment
Post a Comment