Kiasi
cha Waislamu milioni mbili kutoka karibu mataifa yote duniani
walikusanyika katika mlima Arafat nchini Saudi Arabia hapo jana,
wakijiunga pamoja katika imani yao ya haja ya kuitakasa kiroho mwanzoni
mwa hija ambayo hujafanyika kila mwaka. Katika eneo hilo la mlima
Arafat, ambako kuna nguzo zinazoashiria mahali pa mlima wa toba,
unaotambulika kwa lugha ya Kiarabu kama Jabal al-Rahma. Ni muda muhimu
katika ibada ya Hija wakati waumini wakiwa katika mlima Arafat wanaamini
kuwa milango ya pepondi inafunguliwa kwa maombi kujibiwa na dhambi
zilizofanywa hapo kabla kusamehewa. Mtume Muhamad S.A.W anaaminika kutoa
risala yake ya mwisho katika mlima huo kwa mamia ya maelfu ya waumini
akiwataka waislamu kuwa na umoja. Leo ikiwemo mataifa ya Kiarabu ikiwemo
Saudi Arabia wanasherekea Siku Kuu ya Eid El Haji .Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro







Post a Comment
Post a Comment