Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This


BABA mzazi wa staa wa sinema za Kibongo ambaye pia ni Miss Tanzania 2006/2007 Wema Sepetu, Balozi Abraham Isaac Sepetu ameagwa jana jioni nyumbani kwake Sinza - Mori jijini Dar es Salaam.


Tukio hilo lilihudhuria na viongozi mbalimbali wa kiserikali akiwemo Waziri Mkuu Mstaafu Jaji Joseph Warioba, Getrude Mongela pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Benard Membe na wengine wengi waliofika kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu aliyefariki dunia Jumapili ya wiki iliyopita.


Waziri Membe kwa niaba ya serikali ametoa salamu za rambirambi na kuchangia kiasi cha shilingi milioni 1, “Kwa niaba ya serikali tumechangia kiasi cha shilingi milioni 1. Hata mimi pia nilimfahamu marehemu kwa muda mrefu na alikuwa kiongozi makini, Mungu alilaze roho ya marehemu mahali pema peponi amen,” alisema Waziri Membe.

Mwili wa marehemu unatarajiwa kusafirishwa leo asubuhi kuelekea Zanzibar tayari kwa mazishi.

 

Mh. Jaji Warioba  akisaini kitabu cha Maombolezo leo mchana nyumbani kwa Marehemu Balozi Isaac Abraham Sepetu jijini Dar es Salaam Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh. Bernard Membe akisaini kitabu cha maombolezo leo October 29, 2013 nyumbani kwa marehemu Marehemu Balozi Isaac Abraham Sepetu
Mama Gertrude Mongella akisaini kitabu cha maombolezo kwenye msiba wa Marehemu Balozi Isaac Abraham Sepetu nyumbani kwake Sinza Mori leo October 29, 2013


Mh. Jaji Warioba na  Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa kimataifa Mh. Bernard Membe wakibadilishana mawazo kwenye msiba wa Marehemu Balozi Isaac Abraham Sepetu leo October 29,2013

Baadhi ya viongozi waliofika msibani kwa Marehemu Balozi Isaac Abraham Sepetu


Mtoto mkubwa wa Marehemu Balozi Isaac Abraham Sepetu, Aman Isaac Sepetu akizungumza jambo na mwandishi wa habari,  Mkwaia wa Kuhenga  leo October 29, 2013 nyumbani kwa Marehemu


Wema Sepetu akiwa na simanzi nzito
Mwili wa Marehemu Balozi Isaac Abraham Sepetu ukiwa ndani ya jeneza


Ndugu na jamaa wakiuaga mwili wa Marehemu Balozi Isaac Abraham Sepetu leo nyumbani kwake jijini Dar es Salaam leo October 29, 2013

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa kimataifa Mh. Bernard Membe akitoa salamu za rambirambi kwa familia ya marehemu Balozi Isaac Abraham Sepetu leo nyumbani kwake jijini Dar es Salaam leo October 29, 2013

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top