Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
 
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye  PICHA|MAKTABA
Dar es Salaam. Maelekezo yaliyotolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC), Zitto Kabwe kutaka kusitishwa kwa ruzuku kwa vyama vya siasa nchini kutokana na kutowasilisha taarifa za ukaguzi wa matumizi yake, yamevivuruga baadhi ya vyama vilivyotajwa.
Vyama vya siasa vinaonekana kutoa matamshi yanayolenga kujinasua katika hoja hiyo, vikiwemo vilivyomshutumu Zitto, kuilaumu Serikali na hata vingine vimediriki kutaka ruzuku hiyo ifutwe kwa maelezo kwamba ni ubadhilifu wa fedha za umma.
Juzi Zitto alisema tangu 2009 Serikali ilitoa kiasi cha Sh67.7 bilioni kama ruzuku kwa vyama tisa vya siasa, lakini vyama hivyo havijawahi kuwasilisha taarifa za ukaguzi hesabu zake msajili kama sheria inavyoagiza. Kwa sababu hiyo, Zitto aliamuru Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, kusimamisha utoaji wa ruzuku hadi hapo vitakapowasilisha ripoti ya ukaguzi na makatibu wake wakuu kuhojiwa.
Kwa mujibu wa Sheria namba 5 ya 1992 ambayo ilifanyiwa marekebisho ya Sheria namba 7 ya 2009, Vyama vya Siasa vinawajibika kuwasilisha hesabu zake kwa CAG na ofisi hiyo inaweza kuamua kuzifanyia ukaguzi yenyewe au kuteua mkaguzi.
Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh aliwahi kusema kuwa utaratibu ambao umekuwa ukitumiwa na vyama hivyo kwa kuteua kampuni binafsi siyo sahihi na ni kinyume cha sheria.
“Kwa mujibu wa kifungu cha 14 cha Sheria ya Vyama vya Siasa, vyama vinatakiwa viwasilishe hesabu kwa CAG, ndipo tuzikague au tuamue kampuni ya kufanya ukaguzi huo, sasa wao walichagua kampuni binafsi moja kwa moja zikawafanyia ukaguzi,” alisema Utouh wakati akitangaza kuthibitisha ubora wa hesabu za vyama vitano vilivyoshiriki kwenye Uchaguzu Mkuu wa 2010.
Mwenyekiti wa Democratic Party (DP), Mchungaji Christopher Mtikila alipendekeza kufutwa kwa ruzuku hiyo kwa vyama vya maelezo kuwa ni inawanyonya wananchi.
“Badala ya kuvipa vyama vya siasa ruzuku, tuelekeze fedha hizo kwenye miradi mingine ya maendeleo,” alisema Mtikila huku akiahidi kwamba chama hicho kitawasilisha kwa Msajili wa Vyama vya Siasa taarifa yake ya fedha iliyokaguliwa katika kipindi cha wiki mbili kuanzia sasa.
CCM wang’aka
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimemshambulia kiongozi huyo, huku kikisema kuwa Zitto ambaye ni Naibu Katibu Mkuu wa Chadema anapaswa kushughulikia matatizo yaliyopo katika chama chake kwanza kabla ya kuzungumzia matatizo katika vyama vingine vya siasa.
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alisema chama hicho hakihusiki na agizo la PAC la kusimaishiwa ruzuku ya kila mwezi, kwani hesabu zake zimekuwa zikifanyiwa ukaguzi. Alisema CCM ipo tayari kwenda mbele ya PAC kikiwa na hesabu zilizokaguliwa na wakaguzi wa nje, Shirika la Ukaguzi la Taifa (Tanzania Audit Corporation - TAC) kuanzia 1977/1978 hadi 2010/2011.
“Januari 29, mwaka huu niliandika barua yenye kumbukumbu namba CMM/F. 20/80/89 ili kuwasilisha rasimu ya hesabu za mwaka wa fedha 2011/2012 lengo likiwa CAG atupangie siku ya TAC kutukagua,” alisema Nape na kuongeza: “Hesabu zilizokaguliwa na wakaguzi wa nje TAC ambazo ni za 2009/2010 na 2010/2011 tayari ziliwasilishwa kwa CAG.” BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top