Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Katika hali isiyokuwa ya kawaida,babu wa miaka 78 amembaka mjukuu wake mwenye umri wa miaka 14 (majina yamehifadhiwa) mwanafuzi wa darasa la tano huko Mlandizi mkoa wa Pwani.

Akisimulia tukio hilo kwa mtangazaji wa Radio Times Fm, Edson Mkisi Jr, Binti huyo alisema Babu yake alikuwa akimuingilia mara kwa mara wakati bibi yake akiwa hayupo na kumpa kiasi cha shilingi elfu mbili (2000/=) kama malipo ya alichokifanya na kumsihi asije kumwambia bibi yake.
Taarifa za sasa na zilizothibitishwa na binti mwenyewe pamoja na bibi yake zinadai kwamba, binti huyo kwa sasa ni mjamzito wa miezi mitatu na hakuna mpango wa kuitoa mimba hiyo kwa kuwa si siri tena.


Mtangazaji wa kipindi cha Hatua Tatu ya Times fm, Edson Mkisi Jr (aliyevaa fulana ya njano) akiendelea na mahojiano na Babu.

Tayari uongozi wa shule aliyokuwa akisoma binti huyo umemuandikia barua babu wa binti huyo pamoja na uongozi wa serikali za mitaa kwa ajili ya kufika shuleni hapo kwa ajili ya mahojiano zaidi. Kwa sasa binti huyo hajakanyaga shuleni kwa zaidi ya miezi miwili hasa baada ya kugundua amenasa mimba ya babu yake.

Akijibu tuhuma hizo, awali babu huyo aligeuka mbogo na kukanusha tukio hilo na kudai kwamba binti huyo alikuwa na tabia ya kwenda disco na ndipo alipopatia mimba hiyo. Hata hivyo, baada ya kubanwa sana babu huyo alimua kuweka ukweli hadharani na kukiri mimbo hiyo ni yake.
"Kwa kweli ibilisi alinipitia jamani naomba hata kama serikali itanifunga inifunge kifungo cha nje kwa sababu mimi ndio kila kitu pale nyumbani....ni ibilisi tu kwani nililalanae mara moja tu na yeye ndio alinishawishi baada ya kuingia chumbani kwangu wakati ametoka kuoga na mimi kuamua kumpakata na ndio mimba ameingia ingawa sikumuumiza wala kumchana," alijitetea babu huyo mbele ya mkewe kipenzi.


                          Binti aliyepewa ujauzito na babu

 
                          Bibi, Babu na mjukuu aliyepewa ujauzito

                                          Binti akisimulia mkasa

            Mashuhuda hawakuwa nyuma kushuhutia tukio hilo.
Aidha, taarifa toka kwa vyanzo vya kuaminika vilidai kwamba babu huyo alishakamatwa na kupelekwa katika kituo cha polisi Mlandizi kwa ajili ya hatua zaidi ya kisheria.  

                                Chanzo:http://mamuafrica.blogspot.com/

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top