Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This


clip_image002
Msanii wa Muziki wa Bongo Fleva ambaye anafanya Vizuri sana na Stayle yake ya Bongo Bolingo Hamisi Ramadhani Muite H-BABA. Ameamua kutoa kauli yake juu ya swala zima la Kufuturisha ambalo limechukua nafasi katika kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani,

H-Baba ameamua kutoa kauli hiyo baada ya kuona watu wanafanya mambo hayo kinyume na Taratibu za Misingi ya Dini,
"Nawapongeza kwa wale wanaoenda kufuturisha watoto Yatima na waendao kufuturisha Misikitini nawapa pongezi sana kwasababu wanapata dhawabu kubwa sana kuliko wale wanaoalika watu wasioeleweka majumbani kwao alfu wanafuturisha alfu usifanye hivyo kutaka sifa unawaita wandishi wa habari nyumbani kwako ili watu wajue, inakuwa siyo swala la msingi.
clip_image001
Sisi watoto wa kiislamu sifa na Mwezi wa Ramadhani ni vitu viwili tofauti tusitake sifa kuonekana wasafi au kuonekana Bora katika kipindi hiki, inabidi sisi wote turudi nyuma na kuacha maovu yetu yote tulikua tukifanya, kama unafanya jambo lako nenda  msikitini utawakuta watu ambao wako pale kwa ajili ya swala toa msaada wako pale au futurisha pale, Utapata dhawabu kubwa sana.
Lakini uanapokuwa nyumbani kwako ukaalika wasanii wenzako watakuja lakini kumbuka wengine  hawajafunga,  mwingine katoka bar, Mwingine kasuka, Mwingine kavaa Heleni mwingine kavaa hiki na hiki haiswii kwa sisi watoto wa Kiislamu, Tusitake sifa sisi wasanii tumekuwa wataka sifa.

 
Leo umesikia Flani kafuturisha eti na wewe kesho yake unaamka na mimi nafuturisha jamani tusifanye kama kamchezo huu ni mwezi wa Ramadhani tuache sifa, Mimi mbona nimefuturisha nani anae jua? kufuturisha ni wewe na ndugu zako na marafikizako wa karibu, siyo leo nafuturisha Mwandishi Flan Njoo unipige picha njoo unimulike Watanzania waone, wewe ndugu yangu mambo hayaendi ivyoo bwana haiswii maana lazima tambiane ukweli unapofanya jambo baya mwezi huu wa ramadhaniclip_image001[4]
Kwanza wewe Mtoto wa kiume Haujaoa unalala na mwanamke haujamuoa je inaswii..? pia mtoto wa kike unalala na mwanamume hajakuoa je inaswii..? jamani tusichezee Dini hiki siyo kipindi cha kufanya mabo yetu kutafuta sifa,huu ni muda wa kutubu, muda wa kumrudia mola pia ni muda wa kujisafisha.
 
Me nimeoa mke wangu ananipikia ftari vizuri nafunga na mpaka kwa sasa kishavu kinatoka,Nafuturisha watu wanakuja kwangu wanafuturu lakini siyo kwa sifa sasa mnaita mpka TV, Magazeti na Redio aaah jamani nani wewe? sifa za nini kipindi hiki ? unatubu nini sasa? jamani wasanii wenzangu nawasii tuache sifa namaliza kwa kusema KWA ALLAH HAKUNA SIFA" alisema H-BABA

                        ANGALIA VIDEO CHINI


Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top