Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This


WENGI walitarajia mke wa Rais wa Marekani, Michelle Robinson Obama alivyowasili Bongo juzi angekuwa amevaa gauni la kitenge cha wax, lakini sivyo, ‘first lady’ huyo aliwashangaza wengi baada ya kushuka kwenye Ndege ya Air Force One akiwa na gauni jepesi tu.

Michelle Robinson Obama akiwa na Mama Salma Kikwete baada ya kuwasili nchini.


Michelle aliwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere siku hiyo kwa sababu ya ziara ya siku mbili ya mume wake ambaye ni Rais wa Marekani, Barak Hussein Obama Jr.

KUMBE MSHONO WA GAUNI UNA JINA
Mara baada ya kukanyaga ardhi ya Bongo, baadhi ya watu, hasa wadada wa mjini waliokuwepo uwanjani walisema gauni alilovaa Michelle linajulikana kwa jina la ‘sindirela’ 
“Ah! Mke wa Obama amevaa gauni la sindirela jamani, lile gauni ndiyo habari ya mjini kwa sasa. Kumbe na yeye wamo. Mimi nilijua atapigilia gauni la kitenge cha wax kumbe,” alisema mwanadada mmoja aliyevaa suruali ya ‘jinzi’ na fulana ya kijani maarufu kwa jina la ‘form six’.

Michelle akiwa ndani ya jiji la Dar.

Katika hali ya kushangaza, mmoja wa wadada waliokuwa pamoja na huyo aliyelitaja jina gauni hilo alisema atakata kitambaa kama cha Michelle hata kama kitakuwa cha rangi tofauti na kushona mshono wa sindirela.
Michelle mwenye mabinti wawili, Malia na Sasha alionekana ni mwanamke ‘simpo’ kwa vazi hilo na viatu alivyovaa licha ya kwamba huenda ni vya bei mbaya.
Baadhi ya watu walisema viatu hivyo havipatikani kokote kwenye maduka ya Kariakoo jijini Dar, labda maduka ya katikati ya jiji hasa yale ya Mtaa wa Samora. 

HALI YA HEWA YAMPA WAKATI MGUMU
Hata hivyo, hali ya hewa ya siku hiyo ilimpa wakati mgumu Michelle kwani kutokana na ulaini wa kitambaa, gauni lake kila wakati lilikuwa likiashiria kupeperuka na hivyo kumfanya awe makini kulithibiti.

...akitembea sambamba na Mama Salma.

AINGIA OFISI ZA WAMA BILA ULINZI WA KWAPANI
Katika hatua nyingine siku hiyo, baada ya mumewe Obama kutinga ikulu, Michelle alikwenda kwenye Ofisi za Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (Wama) inayoongozwa na mke wa Rais Kikwete, Salma Kikwete zilizopo mjini.
First lady huyo alishuka ndani ya gari lenye rangi nyeusi na vioo vya giza na kuelekea mlango mkubwa wa ofisi hiyo ambapo mwenyeji wake, mama Salma alikuwa akimsubiri.
Tofauti na inavyokuwa kwa wakubwa wengine, Michelle alionekana kutembea peke yake (bila ulinzi wa kwapani) huku walinzi wake wakiwa mbali naye wakiwa wamesimama wakiangalia pembeni.
Ulinzi wa Kimarekani ni wa kumwacha kiongozi kuwa mwenyewe bila kumsonga huku walinzi wakiwa mbali wakiangalia usalama zaidi mbali na alipo anayelindwa. 
Waliompokea Michelle kwenye taasisi hiyo ni pamoja na mke wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin William Mkapa, mama Anna Mkapa na wasaidizi wengine katika taasisi hiyo.

Michelle Obama na mumewe wakiingia kwenye ndege tayari kwa safari ya kurudi Marekani.

MUMEWE AWA KIVUTIO, ABONGA KISWAHILI
Katika ziara hiyo, Rais Obama alikuwa kivutio kikubwa baada ya kushuka Bongo hasa kutokana na mwendo wake wa kuvuta kwa mbali mguu mmoja.
Wabongo waliowahi kufika Marekani na waliokuwepo uwanja wa ndege siku hiyo walisema mwendo wa Obama hupendwa kutumiwa na ‘vijana wa mjini’ wa nchi hiyo hususan ‘maniga’.
Sauti yake wakati wa kutoa hotuba ikulu nayo iliwavutia wengi waliokuwa wakiamini ingebadilika tofauti na anavyokuwa nchini mwake.
“Kumbe jamaa sauti yake ni hiyohiyo, ni nene, kwa kweli inavutia kwa rais, mi nilijua ni kwa Marekani tu,” alisema Mbongo mmoja alipokuwa akiangalia hotuba hiyo kupitia runinga ambapo pia alimpongeza kwa uwezo wake mkubwa wa kujibu maswali ya waandishi wa habari.

Michelle Obama na mumewe wakiaga.

Kivutio kingine kilichoonekanna kwa Obama ni kitendo cha kuwasalimia mapaparazi kwa Kiswahili kabla hajaanza ‘kuwahubiria.’
Obama pamoja na kuzungumza ‘kimombo’ alisalimia kwa kusema: habari zenu. Alipomaliza hotuba yake alisema: Asante. 
Katika kuonesha huenda kiongozi huyo anakijua vyema Kiswahili hata alipokuwa nchini Afrika Kusini alitumia neno asante kuwashukuru raia wa nchini hiyo. 

AANIKA HISTORIA YA BABA YAKE
Hakuna jambo lililowavutia Wabongo kama pale Rais Obama aliposema kwamba baba yake (marehemu Obama) alikuwa Mkenya lakini muda mwingi aliutumia Tanzania licha ya kwamba hakutaja sehemu aliyokuwa akifikia mzee huyo.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top