Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
John-Mnyika

Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa CHADEMA, John Mnyika (MB – Ubungo) amesema chama chake kitatoa mkanda wa video unaoonesha ulipuaji na shambulio lililofanyika katika viwanja vya Soweto (AICC) Arusha siku ya Jumamosi, Juni 15, 2013 wakati wa kufunga kampeni za uchaguzi wa udiwani za Kata za mkoa huo.

Mnyika amesema wataukabishi si tu kwa Polisi baada ya kupata ushauri wa kisheria, hasa baada ya Polisi kuonyesha kutokuwa na nia nzuri, bali watauweka hadharani, “kabla ya polisi kujua kuwa CHADEMA ina mkanda, polisi walishahisi kuna recording imefanyika, kwa hiyo wakaanza kutafuta watu wanaodaiwa kuwa wamerekodi na kuwakamata na kuwapiga na kuwatesa, badala ya kuwachukulia kama raia wema wa kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi. Katika mazingira haya ya jeshi la polisi, kuonekana kwamba linataka ushahidi siyo kwa njia njema, timu yetu iliyoko Arusha, ikiongozwa na Mwenyekiti, imeamua kwamba, kabla ya kutoa huo mkanda kwa umma, tukae na jopo letu la wanasheria. Mkanda huu tutautoa, wazi kabisa, ili Watanzania na Dunia ijue kwamba Serikali hii inatumia umwagaji damu kubaki madarakani, halafu inageuza kuwa CHADEMA ndiyo inayofanya hivi

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top