Waigizaji waliopo juu kwenye kiwanda cha filamu nchini, Vincent Kigosi ama Ray na mrembo Jacqueline Wolper , wapo location wakishoot movie yao mpya ambayo bado hatujaweza kupata jina lake mpaka sasa kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wetu.
Katika picha walizoziweka kwenye akaunti zao za mtandao mmoja wa kijamii nchini inaonekana wanaigiza kama mke na mume.
“Siye tena kazini new movie, mke wa mtu me hapa nacheza.me en broo ray mwenyezi mungu kua nasi mwanzo hadi tumalize inshaalah ,” ameandika Wolper kwenye moja picha hizo.
Filamu hii inatengenezwa na kampuni ya RJ
company iliyoshinda tuzo ya best production house kwenye tuzo zilizotolewa na
kampuni ya usambazi wa filamu Tanzania Steps Entertainment Limited
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Post a Comment
Post a Comment