BEKI Eric Abidal jana alihitimisha miaka yake sita
Barcelona na kufanyiwa tafrija nzuri ya kuagwa ndani ya Uwanja wa Nou
Camp.
Beki huyo Mfaransa mwenye umri wa miaka 33, ambaye
alirejea uwanjani baada ya kupona matatizo ya ini, alipewa jezi ya fremu ya
Barca iliyoandikwa 'Merci Abi' na akanyanyuliwa juu na wachezaji
wenzake.
Cesc Fabregas, anayetakiwa na Manchester United,
Manchester City na Arsenal, na David Villa, anayetakiwa na The Gunners na
Tottenham, wanaweza kuwa walicheza mechi yao ya mwisho katika ushindi wa 4-1
dhidi ya Malaga.
Abidal aliingia uwanjani akitokea benchi dakika ya 75
kuwaaga mashabiki baada ya kutangaza hatasaini tena msimu mwingine mapema wiki
hii huku akibubujikwa na machozi.

Abidal akiwa na fremu ya jezi
aliyopewa
Abidal alisajiliwa kama mchezaji huru kutoka Lyon mwaka
2007 na amecheza karibu mechi 200. Katika miaka yake sita ameshinda mataji manne
ya La Liga, mawili ya Ligi ya Mabingwa,
mawili Kombe la Mfalme, matatu ya Super Cup ya Hispania na mawili ya Klabu
Bingwa ya Dunia ya FIFA.
Pia aliingizwa kwenye timu ya UEFA ya mwaka 2007 na
akashinda tuzo ya beki bora La Liga mwaka 2011.
Cesc Fabregas alifunga bao
zuri jana ambalo linaweza kuwa bao lake la mwisho
Mchezaji anayetakiwa na Spurs
na Arsenal, David Villa pia alifunga
Abidal akiwa na mpwa wake,
Gerard, ambaye alimsaidia wakati wa tiba
Kimataifa alikuwemo kwenye kikosi cha Ufaransa
kilichoshika nafasi ya pili katika Kombe la Dunia mwaka 2006 na amecheza jumla
ya mechi 61 katika timu hiyo. Pia ameshinda mataji matatu ya Ligue 1 akiwa na Lyon.
Katika Mkutano na Waandishi wa Habari mapema wiki hii
alisema: "Ningependa kubaki, lakini lazima nikubaliane na uamuzi wa klabu
(kutoniongezea mkataba).
"Lengo langu ni kuendelea kucheza na sijabadilisha
mawazo, suala ni afya. Ni siku ngumu sana kwangu,".

Eric Abidal alimwaga machozi
alipokuwa anatangaza kuondoka kwake
"Nimecheza hapa kwa miaka sita, na umekuwa uzoefu
mkubwa katika maisha yangu. na nilikuwa nina malengo mawili: kupambana mabinti
zangu wakue na kucheza tena.
"Nataka kuwashukuru mashabiki wote wa klabu ambao
walinisapoti.
"Timu ni familia yangu ya pili. Tumepitia mengi pamoja
na nitakumbuka hii daima. NakwendaI,
nitahakikisha narudi,"alisema.
Fabregas na Villa wote wanaandamwa na tetesi za
kuondoka kwenda kucheza Ligi Kuu England na kiungo wa zamani wa Arsenal,
anatarajiwa kuwa na mazungumzo na kocha Tito Vilanova wiki
ijayo.
Aliingia dakika ya
75


Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro







Post a Comment
Post a Comment