Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This


MSANII wa muziki wa kizazi kipya nchini, Abdukarim Kiba ‘Abdukiba’ yuko mbioni kuachia kibao chake kipya kinachokwenda kwa jina la ‘Siamini’ hivi karibuni.

Akizungumzia kibao hicho, Abdukiba alisema, yupo katika hatua za mwisho za uandaaji wa wimbo huo na ataisambaza katika vituo mbalimbali vya radio mwishoni mwa wiki hii.

Alisema katika wimbo huo, kuna baadhi ya wasanii wa muziki wa kizazi kipya watasikika, ambao hajapenda kuwataja ili kuwapa mtihani mashabiki wake kujiuliza nani ambaye kamshirikisha.

“Sipendi kusema nimemshirikisha nani katika wimbo huo, ila ningependa mashabiki wangu wakae mkao wa kula kwa ajili ya wimbo huo, najua wengi wataupenda kulingana na jinsi ulivyo tofauti na nyimbo nyingine,” alisema Abdukiba.


Mbali na ‘Siamini’, Abdukiba alishawahi tamba na vibao kama ‘Kizunguzungu’, ‘Huyo si demu’ ‘Kidela’ na nyinginezo ambazo zinafanya vizuri katika tasnia ya muziki wa kizazi kipya.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top