MSANII wa
muziki wa kizazi kipya nchini, Abdukarim Kiba ‘Abdukiba’ yuko mbioni kuachia
kibao chake kipya kinachokwenda kwa jina la ‘Siamini’ hivi
karibuni.
Akizungumzia
kibao hicho, Abdukiba alisema, yupo katika hatua za mwisho za uandaaji wa wimbo
huo na ataisambaza katika vituo mbalimbali vya radio mwishoni mwa wiki
hii.
Alisema
katika wimbo huo, kuna baadhi ya wasanii wa muziki wa kizazi kipya watasikika,
ambao hajapenda kuwataja ili kuwapa mtihani mashabiki wake kujiuliza nani ambaye
kamshirikisha.
“Sipendi
kusema nimemshirikisha nani katika wimbo huo, ila ningependa mashabiki wangu
wakae mkao wa kula kwa ajili ya wimbo huo, najua wengi wataupenda kulingana na
jinsi ulivyo tofauti na nyimbo nyingine,” alisema
Abdukiba.
Mbali na
‘Siamini’, Abdukiba alishawahi tamba na vibao kama ‘Kizunguzungu’, ‘Huyo si
demu’ ‘Kidela’ na nyinginezo ambazo zinafanya vizuri katika tasnia ya muziki wa
kizazi kipya.
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Post a Comment
Post a Comment