Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Mrisho Ngasa akiongea na waandishi wa Habari leo makao makuu ya klabu ya Yanga baada y akutambulishwa rasmi jana
DAIMA MBELE NYUMA MWIKO  (DMNM)
EVER FORWARD BACKWARD NEVER (EFBN)
Mrisho Ngasa akikabidhiwa jezi ya klabu ya Yanga na katibu mkuu Lawrence Mwalusako
Amesaini kadandalasi ya miaka miwili kuichezea yanga akitoka kwa wapinzani wao simba 
MRISHO Ngassa jana Jumatatu kafunga kazi.Katambulishwa mbele ya waandishi wa habari rasmi kwamba yeye ni mchezaji wa Yanga na kaibusu jezi ya Yanga mbele yao. Kama kusaini alishasaini zamani kabla Sir Alex Ferguson hajastaafu Manchester United au kabla Francis Cheka hajapigana na Thomas Mashali
Amefanikisha alichokuwa anakitaka. Siku zote anataka kucheza Yanga. Ndio timu ya damu yake. Ndio timu ya akili yake. Ndio timu ya ngozi yake. Ndio timu ya nywele zake. Haifikirii West Ham, Libolo, El Marreikh, Seattle Sounders wala Manchester United. Lugha rahisi ni kwamba amepata alichotaka. Hongera nyingi kwa Ngassa.
Kikubwa zaidi ni kwamba wakati utatuambia. Mungu akitupatia pumzi mpaka nyakati hizo tutakutana uzeeni na kujadili kwa kirefu majuto ya maisha yetu. Wakati huo hatutotaka kusikia lawama wala manung’uniko na masikitiko ya kukosa kucheza Ligi Kuu England. Tutakuwa bize na wachezaji wengine.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top