Hashim Lundenga.Baada ya shutuma za rushwa ya ngono kuzidi kwa waandaaji wa shindano la Miss Tanzania, uongozi unaosimamia shindano hilo umesema kama kuna mrembo yeyote ambae amewahi kuombwa rushwa hiyo ya ngono ajitokeze.
Mkurugenzi Hashim Lundenga amesema “kuna kushutumiwa kwamba tunachukua
rushwa ya ngono kutoka kwa Wasichana kitu ambacho sio kweli, hakuna
msichana aliesema ameingia kambini au ameshinda kwa sababu ametoa rushwa
ya ngono, katiba yetu inakataza kabisa yeyote kujihusisha na hilo”
.Toka Miss Tanzania ianze 1994 mpaka sasa kuna kesi zisizozidi nne za
wazazi waliokuja kuwaondoa watoto wao kwenye kushiriki mashindano hayo
baada ya kupata taarifa mbaya kuhusu hizo kashfa za ngono.
Moja ya kesi hizo ni pamoja na ya Mchungaji aliemuondoa mwanae baada ya
kupewa ubalozi wa kinywaji chenye kilevi, mrembo mwingine alikua Nadya
aliekua masomoni Chuo kikuu familia yake ilikataa kabisa mtoto wao
kushiriki.
.Lundenga amesema kuna wazazi wengine ambao walieleweshwa na wakaelewa
akiwemo Mzee Muhere ambae aliposikia mtoto wake ameshinda Miss Kinondoni
aliwapigia kelele sana lakini akaeleweshwa akaelewa na sasa mtoto wake
anamiliki kampuni kubwa na anaendesha maisha vizuri kuliko baba yake
alivyodhani.
Kwa kumalizia, Lundenga amekiri kwamba wanao utaratibu, sheria na kanuni
kwenye katiba yao ambayo imepitishwa na Serikali ikiwa na maagizo
mablimbali ikiwemo marufuku ya kiongozi yeyote kuomba rushwa ya ngono.
Pamoja na kuzushiwa hizo kashfa, amesema idadi ya Warembo wanaotaka
kushiriki haijapungua bali imeongezeka kwa sababu Wasichana ndio
wanazidi kujitokeza.
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Post a Comment
Post a Comment