Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

MTU anayedhaniwa kuwa ni mgonjwa wa akili, amembaka na kumuua kwa kumpiga fimbo kichwani na usoni kisha kumnyonga shingo mama yake mzazi mwenye miaka 73, mkazi wa Kijiji cha Ibungila wilayani Rungwe, mkoani Mbeya.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi, alimtaja mtuhumiwa kuwa ni Kiswigo Anganisye (33), mkazi wa kijiji hicho.
Alisema kuwa, tukio hilo limetokea juzi, majira ya saa 6:30 usiku, ambako inadaiwa kuwa, kabla ya kuuawa, marehemu pia alibakwa na mtuhumiwa.
Hata hivyo, Kamanda Msangi alisema kuwa, chanzo cha tukio hilo, inadaiwa kuwa ni baada ya marehemu kumpikia mtuhumiwa magimbi badala ya ugali, ndipo alipochukia na kuchukua uamuzi huo na kwamba amekamatwa na anashikiliwa na jeshi hilo.
Na Samwel Ndoni -Mbeya
kama huja like ukurasa wetu wa facebook fanya hivi sasa ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu BONYEZA HAPA

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top