MTU
anayedhaniwa kuwa ni mgonjwa wa akili, amembaka na kumuua kwa kumpiga
fimbo kichwani na usoni kisha kumnyonga shingo mama yake mzazi mwenye
miaka 73, mkazi wa Kijiji cha Ibungila wilayani Rungwe, mkoani Mbeya.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi, alimtaja mtuhumiwa kuwa ni Kiswigo Anganisye (33), mkazi wa kijiji hicho.
Alisema
kuwa, tukio hilo limetokea juzi, majira ya saa 6:30 usiku, ambako
inadaiwa kuwa, kabla ya kuuawa, marehemu pia alibakwa na mtuhumiwa.
Hata
hivyo, Kamanda Msangi alisema kuwa, chanzo cha tukio hilo, inadaiwa
kuwa ni baada ya marehemu kumpikia mtuhumiwa magimbi badala ya ugali,
ndipo alipochukia na kuchukua uamuzi huo na kwamba amekamatwa na
anashikiliwa na jeshi hilo.
Na Samwel Ndoni -Mbeya
kama huja like ukurasa wetu wa facebook fanya hivi sasa ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu BONYEZA HAPA
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro






Post a Comment
Post a Comment